i miss you

 Siku zote kwangu ni sherehe ni wewe unishereheshaye,  ukweli usio na kejeli mapenzi yako yanatii kiu yangu, moyoni mwangu nimeridhia... Nakupenda daima mpenzi!

****


Ahsante Mungu shukrani kwako mama, pongezi kwako mpenzi kuwa wangu mtetezi kwenye jahazi la mapenzi, ufundi na ujuzi unao hasa tuwapo wawili chumbani. Penzi lako halichakai daima huzaliwa jipya.

******

Mapenzi ni upepo, mimi sivumi na kupotea, mapenzi ni mahaba sili nikamaliza, nikimaliza nitakula nini kesho? Nakuahidi kukupenda leo hata kesho ukiwepo na hata usipokuwepo.




Post a Comment

أحدث أقدم