1.PAPARA
wanaume wengi tumekuwa na haraka sana tunapokuwa tukitaka kuaproach hali inayomfanya mwanamke akuwekee ugumu.mfano umekutana na dada mzuri mmesalimiana hapo hapo unamuomba namba yake.mjomba hata akikupa ujue utasumbuka sana kumpata coz atakufikiria sana juu ya uharaka wako.
2.KUJIFAKE
wanaume wengi tumekuwa tukijipandisha au kujionyesha tofauti na hali zetu.ukiwa unaaproach jaribu kuwa real.huwezi kumwambia mdada unafanya kazi benki afu uko na techno
3.KUTOSOMA MOOD YA MWANAMKE
unapomuaproach mwanamke lazma usome mood yake coz sometime unaweza kutoswa coz hujamsoma mwanamke.unamtongozaje mwanamke asubuhi?,,
4.KUMPONDA UR EX LOVER
mwanamke anakuuliza kwanini uko single,unaanza kumponda ex wako kwa maneno ya kashfa hali kama hii inaweza kumtisha kisaikolojia umtongozae.
5.KULALAMIKA
Unamtongoza mwanamke huku unalalamika juu ya mapenzi oooh mara sijawahi kupendwa.mjomba hapo unaonyesha udhaifu wako.UKITULIA NA KUMTONGOZA MWANAMKE BILA KUYATENDA HAYA MBNA UTAMPATA KILA UMTAKAE

Jinsi Ya Kumtext Mwanamke Hadi Akupigie Simu Wa Kwanza

Kutumia sms kuanzia wiki hadi mwezi bila kupiga simu ni VIBAYA. Unahatarisha kuitwa boyfriend wa sms, na labda hautakuwa boyfriend wake wa ukweli. Kuondoa hizi athari unapaswa kutumia maujanja haya matatu.
Mbinu #1: Toa majibu yasiyokuwa moja kwa moja.
Wanawake wanapenda majibu ya moja kwa moja kama wanataka kujua kitu flani kutoka kwako. Mwanamke anaweza kukuuliza “Wewe unafanya kazi gani?” ama “Uko na tatoo kwa mwili wako?” Usijibu maswali haya moja kwa moja. Badala yake mzungushe  kwa kumwambia “Mimi ni jasusi siku za juma halafu wikendi nafanya kazi kwa club kama bausa.” Kama ataudhika na jinsi umekataa kujibu swali lake moja kwa moja, unaweza kumwambia “Nitakwambia tukikutana” ama “Nitakwambia wakati tunaongea kwa simu.”
Mbinu #2: Mtumie meseji ya utani kama hakukujibu.
Kama atashindwa kukutumia meseji baada ya lisaa moja, mwambie “Umefutwa kazi.” Atakupigia na kutaka kujua ni kwa nini umemwambia hivyo na atataka ueleze kwa upana umemaanisha nini.
Mbinu #3: Weka ratiba ya kupiga simu.
Kama mnatext na moto, kama vile anareply texts zako chini ya dakika moja baada ya kumtumia text, katiza maongezi yanu kwa kumwambia “Hey, nataka kwenda, lakini nitakupigia simu kesho jioni.” Kama utafanya hivi vile inavyotakikana atataka akupigie wewe simu na atakuwa active wakati wote.
Wakati unatimiza mbinu hizi, kuna sheria ambazo unahitajika kufanya ili akuheshimu wakati wote.
Sheria #1:  Moja kwa moja – Anapaswa kutuma angalau jumbe mmoja kwa kila jumbe ambayo utamtumia.
Sheria #2: Kama hatajibu meseji yako moja, usimtumie meseji siku nzima. Kama hatajibu meseji yako ya pili usimtumie jumbe wiki nzima.
Sheria #3: Usimtext ukimwambia jinsi unahisi vibaya kwa kuwa anakataa kujibu meseji zako badala yake umpigie simu na umsunze kuhusu simu yake.
Waweza kusema “Hi, najua kuna kampuni ambayo itakulipia bili ya wiki nzima ya mjazo wako wa simu kwa kufanya kazi mfano wa mhudumu wa hoteli. Je unataka nikuunganishe?
Kwa kutumia mbinu hizi tatu + hizi sheria tatu utakuwa uko sawa katika gemu ya kutext.
NB Mbinu hizi zitafanikiwa kirahisi iwapo umejenga tenshen ya kimapenzi kati yako na mwanamke. Hivyo kama unaanza kumtext mwanamke siku ya kwanza mbinu hii haitafanikiwa.

Hatua Za Kumfanya Mwanamke Amuache Mpenzi Wake Aje Kwako

Wakati umekutana na mwanamke mrembo halafu ukapiga naye gumzo zuri, unaweza mwisho kugundua kuwa ana boyfriend. Ama labda una rafiki mwanamke mrembo ambaye tayari ana mpenzi. Kwa njia yeyote ile, kujua kuwa mwanamke amechukuliwa kunaweza kukatiza matumaini. Mwanzo, wanaume wengi hukatizwa tamaa wakati wamezungukwa na wanawake warembo aina hii ambao tayari wameshachukuliwa.
Kukatiza stori fupi, hapa utakuwa umebakishwa na uchaguzi miwili ambayo unapaswa kuchagua ikifikia hapa: unaweza kuamua kuachana naye, ama unaweza kuchukua hatua ya usoni. Sasa hii haimaanishi ya kwamba unapaswa huuvunja uhusiano ambao tayari yuko nao ama tayari anafurahia. Lakini, kama anaonekana kuwa hajapendezwa na mahusiano ambayo tayari yuko, ama umeingiwa na hamaki ya kumtaka awe girlfriend wako, basi kuna hatua kadhaa ambazo unaweza kuzitumia ili umfanye aachane na mpenzi wake na akufuate wewe.
Hatua #1 Chambua mahusiano yako
Kabla kuchukua hatua yeyote lazima uchambue mahusiano yake na wewe. Je anakuchukuliaje? Kama amekuingiza katika himaya ya urafiki, basi tatizo hapa halitakuwa kwa boyfriend wake bali uhusiano wake na wewe wa kirafiki. Wanawake huwa na fikra mbilimbili kabla hawajaanza kudeti marafiki zao wa dhati kwa kuwa hawataki kuharibu uhusiano wao wa kirafiki nao.
Katika kesi nyingine, wanawake wanakuwa marafiki wazuri na mwanaume kiasi cha kuwa hawaingiwi na mawazo ya kuwa wanaweza kuwadeti hata kama wako single. Hii inaweza kuwa kama kesi unayoipitia sahizi. Hili neno ‘friend zone’/himaya ya urafiki linatumika sana na wanaume wengi wanafanya makosa mpaka wanajikuta wameingizwa katika shimo hili ambalo ni vigumu kujinasua – hili jambo liko na linakera sana. Kama umenaswa katika hili jinamizi na ‘friend zone’ na mwanamke unayempenda, basi fanya hima hima ujinasue na ufuate mbinu thabiti ambazo zitakujeuza mwanaume tofauti ambaye anaweza kudeti naye.
Hatua #2 Jifanye kama uko single
Baada ya kuchambua mahusiano yenu, anza kufikiria mambo ambayo munaweza kuyafanya mkiwa pamoja na mambo ambayo hupaswi kufanya akiwa na wewe. Mfano hupaswi kuleta stori za kumhusu mpenzi wake, ili uweze kumsoma kiwango gani ambacho anacho ikija kwa kumpenda mpenzi wake.
Kama hamzungumzii kuhusu mpenzi wake mara kwa mara katika maongezi yenu, basi itakuwa ni ishara ya kwanza kuonyesha kuwa hayuko interested na yeye sana. Hii itakurahisishia kazi kwako kuweza kumnasa kiurahisi. Kile ambacho unahitaji kufanya nikumsuka zaidi, ongea na yeye vile ambavyo anataka uongee naye, na pia mfanye akuone kuwa unavutia kadri wakati unavyosonga.
Hatua #3 Linganisha ustadi wako wa mahusiano
Wakati huu, nni wakati wa kujilinganisha wewe na boyfriend wake kinjia fioa, yaani kujipima uwezo wako na boyfriend wake kichinichini. Kwa kuanza mambo, unapaswa kuongea kuhusu vile ambavyo unaweza kuwa boyfriend mbaya kwa sababu unapenda maisha sana. Mbinu hii ya maongezi ni ya viini macho ambayo tuliieleza kwa kina awali katika machapisho yenu. Huku kutamfanya mwanamke kutaka kujua ni kwa nini unapenda maisha, na ni kivipi utakuwa boyfriend mbaya kwake. Pia katika mazungumzo yako, muelezee ni kivipi unayapenda maisha yako na jinsi unavyoishi. Kufanya hivi kutamfanya mwanamke ajenge picha ya maisha yako akiwa na wewe. Utamsisimua na kumfanya akuone kuwa maisha yako ni ya furaha wakati wote.
Kwa kufuata hatua muhimu, unaweza kuiba atenshen ya mwanamke ije kwako, na kuweza kumuwini mwishowe hata kama tayari ana boyfriend – aminia hili. Pindi utakapofanikiwa, anaweza kukuonyesha hata dalili za kuwa ameanza kufall na wewe na kumuacha mwanaume aliyempenda awali  kabisa…
Upo!

Njia Rahisi Ya Kuchukua Namba Kutoka Kwa Mwanamke Unayemjua

Kuchukua namba kutoka kwa mwanamke ni rahisi zaidi kuliko hata kutamka jina lako. Unachohitajika ni kuenda moja kwa moja kwa mwanamke unayetaka kumuomba namba halafu unamwagiza akupatie. Mara nyingi mwanamke hawezi kukataa kukupatia namba yake unless uwe umemuapproach kwa njia isiyofaa ama hakujui.
Mara ya mwisho mimi binafsi nilichukua namba kwa mwanamke chini ya dakika moja ya kukutana na yeye. Nilikuwa nimeandamana na marafiki zangu halafu mwanamke mmoja akapita kando yetu halafu muda wa dakika nikaamua kumuaproach na kunipatia namba yake ya simu hapo hapo.
Kama bado unatatizika ni njia gani za kuchukua namba ya simu kutoka kwa mwanamke basi fuata maagizo haya ya haraka ambayo nitakuelezea.
#1 Jiamini. Kujiamini ni kitu muhimu. Wakati unapoamua kuapproach mwanamke lazima uwe unajiamini. Utajiamini vipi? Kujiamini ni rahisi. Kile unachohitajika kufanya ni kuweka nia kuwa wakati ambapo utamwaproach mwanamke lengwa basi lazima namba yake ya simu atakupatia. Huko ndiko nikujiamini.
#2 Kuwa na mawazo chanya. Mawazo chanya ni mawazo ambayo yanakubaliana na wewe. Mfano unaweza kuwa unataka kufanya kitu, halafu katika akili yako umeweka dhana ya kuwa kile ambacho unakusudia kufanya basi kitafanikiwa. Haya ndio tunayaita mawazo chanya. Ni dhana ambayo unaamini kuwa itatokezea. Ukiweka mawazo chanya kuwa ukiapproach mwanamke flani na atakupa namba yake ya simu basi bila shaka utafanikiwa. Lakini ukiweka mawazo ya kuwa hautafanikiwa basi kweli hautafanikiwa.
#3 Kuwa mwigo. Wakati mwingine inakuwa vigumu kabisa kwa wanaume flani kuongea na mwanamke. Inakuwa vigumu zaidi kuomba namba kutoka kwa mwanamke. Njia rahisi ya kutatua shida hii haraka ni kuigiza. Kuomba mwanamke namba haichukui zaidi ya dakika mbili, hivyo unaweza kuwa mwigo. Unaweza kuigiza vile rafiki yako anavyoomba namba ya simu ama unaweza kufanya mazoezi kivyako kabla kumuapproach mwanamke kumuomba namba ya simu.
#4  Relax. Wakati unapoach mwanamke lazima uwe umetulia. Punguza wasiwasi, toa kijasho chochote ambacho uko nacho, pumua kiutulivu na uondoe ubabaifu wowote ulio nao. Hii itakusaidia kwa kuwa ukiwa umerelax utakuwa na nafasi nzuri ya kukumbuka mambo ambayo umeyapanga kumwambia mwanamke flani. Hivyo ni muhimu kurelax kabla ya kuchukua approach yeyote.

 Njia nzuri ya kumuapproach mwanamke

Njia rahisi ya kuomba namba ya simu kutoka kwa mwanamke ambaye unamjua na anakutambua ni ile ya moja kwa moja. Ukimwona anatembea mtaani halafu wewe umesimama na marafiki zako, mwanzo hakikisha umefuata masharti tuliyoyaeleza hapo juu; jiamini, relax, mawazo chanya na mwigo. Nenda moja kwa moja na umwambie hivi:
“Mambo Mamito. Niko na ishu flani nataka kukuambia lakini sahizi naona si wakati mzuri wa kukuambia… Nipatie namba yako ya simu nitakupigia simu usiku.”
ama
“Mambo Mamito. Napatie namba yako ya simu nataka kukupikia simu jioni nikwambie kitu flani”
Hii ndio njia ya moja kwa moja. Mwanamke wa kawaida, ambaye anakutambua hawezi kukataa kukupatia namba yake ya simu. Mwanzo unaweza kuwa na bahati ya kuwa huyu mwanamke alikuwa inteested na wewe tangu kitambo lakini anashindwa jinsi angeweza kuwasiliana na wewe.
Kama ni mwanamke ambaye humjui na hakujui, basi ni vyema kwanza ujitambulishe ili akufahamu. Si lazima uchukue namba yake ya simu siku io hio bali unaweza kungojea muda mpaka mzoeane.
Wanaume wengi wanatatizwa na tatizo la kutojiamini na woga. Lakini naamini kama unaweza kutatua mambo hayo mawili basi kazi yako itakuwa rahisi.

Mbinu tatu (3) za kumtongoza msichana ili akubali mapema

Miongoni mwa maswali ambayo huwachanganya wavulana wengi ni pamoja ni kwa jinsi gani anaweza kumtongoza msichana na hatimaye akakubali. Wengi wao wanakuwa hawana ile nguvu ya kujiamini  ya kumtongoza msichana huyo macho kwa macho, wengi wao utawasikia ooh samahani naomba namba yako.
Sasa ili kuwaponya madomo zenge walio wengi hii ndiyo tiba ya kumtongoza mrembo yeyote hatimaye akakukubali.
1. Usimfanye ajue unampenda kwa dhati.
Wanaume wengi huwa wanafanyaga kosa hili kubwa . Wanawaambia wanawake wanawapenda au wanahisia za kimapenzi kwao . Ni kweli unampenda , anajua hivyo tayari . Au hajui ? Unampigia simu kila saa , mnataniani kimapenzi na anaona uhusiano wenu kabisa .
Kwahiyo japokua anahisi unampenda , usije kuonyesha hivyo kwani anahitaji kusikia kutoka kwako ili ajihakikishia hisia zake . Chukulia poa na usifunguke kuhusu hisia zako kwake , kitendawili alichonacho ndicho kitamfanya azidi kukunata na kutaka kujua mwisho wa mambo .
2. Ishi Maisha mawili
Unapoongea nae usiku , mwaga sera zako na funguka kuhusu mambo ya mapenzi sema mkikutana ana kwa ana mchana usiongelee mambo ya mapenzi kabisa labda aanze yeye na hivyo kumaanisha ashaingia line na anapenda maongezi hayo .
Pia epuka kuongelea kuhusu mambo yenu ya kimapenzi mnapokua na marafiki wengine bali fanyeni hivyo mkiwa wawili . Kwa kufanya hivyo unamfanya aamini kuna uhusiano motomoto wa siri unapikika kati yenu
3. Kuwa karibu na mtu huyo.
Siku zote , kama unataka kumtokea msichana njia muhimu kabisa ni kuweza kumjua kwa undani .Usikurupuke kurupuke tu ukaanza kutongoza , msichana ataogopa au atakuona mtu rahisi kua nae na mwisho wa siku utaishia kumboa tu .
Ongea nae na upate kumjua vizuri . Mtumie message na usiwe na mzuka , mfanye awe kama rafiki kwanza . Usimtokee kwanza sema pia usisubiri sana maana ataanza kukuchukulia poa .
Ukitumia mbinu hizo tatu nina imani kubwa ni lazima msichana huyo utampata tu.

Sheria Za Kufuata Unapomtumia Meseji Uliyemzimia

mepewa nambari ya simu na mwanaume/mwanamke unayemzimia na hujui aina gani au ngapi za meseji unazotaka kumtumia? Cheza kwa ujanja ukitumia sheria hizi ambazo ni lazima yeyote anafaa kutumia ikija maswala ya kumtext yeyote aliyemzimia.
1. Mtext unayemzimia kwa maswali rahisi
Kama unamtaka yule uliyemzimia ajibu texts zako, lazima utoe sababu muhimu kwake kujibu texts zako. Unaweza kuanza kumtext kwa kumuuliza anafanya nini muda huo ama unaweza kumtext na kitu ambacho mlikuwa mkifanya pamoja wakati uliopita. Mfano unaweza kumtext ‘Ile story ya kuenda kumtembelea binamu yako ilifikia wapi?’
2. Usingojee ajibu meseji ukiwa hapo
Iwapo amejibu text yako kwa haraka ni vyema. Lakini kama atachukua muda mwingi, usijisumbue kamwe kukaa karibu na simu. Tafuta kazi nyingine ile ujikeep buzy usijishughulishe na kufikiria meseji uliyomtumia.
3. Usimtext unayemzimia meseji nyingi wakati mmoja
Usijaribu kutuma zaidi ya meseji moja kabla hajakujibu. Hii itaondoa ile hisia ya kuonekana kama mtu mwenye tamaa ama kuonekana kama una ajenda chafu. Hii itajitokeza iwapo kama huyo unayemzimia hujakuwa na mazoea naye.
4. Mazungumzo yenu yaendelee…hadi pale kikomo
Iwapo maongezi yenu yanaendelea vizuri basi ni vyema. Hakikisha ya kuwa usipitishe maongezi yenu mpaka yaingie kitengo cha kuboesha. Ukiona unayemzimia anachukua muda mrefu kujibu texts zako ama kujibu kwa neno moja moja, basi fahamu ya kuwa maongezi yenu yamefika kituo na unafaa kusmamisha texts zenu hadi siku nyingine.
5. Endeleza maongezi binafsi
Kutumia mtu meseji ni rahisi sana kwa kuwa inatoa tenshen na wasiwasi. Pia meseji husaidia mtu kujieleza zaidi. Lakini unafaa kufahamu ya kuwa meseji pekee haziwezi kumshawishi mtu kwa kiwango kikubwa hivyo unafaa ufuatilie wewe binafsi ukutane na unayemzimia ili uendeleze maongezi yenu.
6. Tafuta ishara kubwa kama unayemzimia hajakupenda
Je wewe ni yule ambaye wakati wote unaanza kumtext huyo uliyemzimia?  Je unayemzimia ni yule ambaye anakutumia text wakati wa shida na hawezi kukutext wakati mwingine?  Hii ni dalili ya kuonyesha ya kuwa yule unayemtext kwa kawaida anafanya hivyo ili kuondoa uchoshi kwake ama anafanya hivyo kukuonyesha tu heshima kwako.
Ukiona mtu anamiliki aina hii ya tabia basi ni ishara ya kukuambia ujipatie shughli na utafute kwingine.

Jinsi ya kuondoakana na aibu hatimaye uweze kujiamini

Wakati mwingine wanadamu tumeubwa na sura za aibu aidha kwa kujua au kwa kutokujua pia. Lakini wapo watalamu mbalimbali wa masuala ya saikolojia ambao wameleza kwa kina kuhusu namna ambavyo unaweza kuondokana na tatizo hili.
Na zifutazo ndizo njia za kuondokana na aibu:
1. Fanya kitu unachokiogopa.
Kama wewe umeumbwa na hulka hii ya aibu basi unatakiwa kuanza kitu kitakachokufanya uwe na aibu hiyo, kama huwa unaogopa kuongea kwa watu maana yake hicho ndicho unachokiogopa, hivyo ili kuweza kujinasua katika aibu hii basi unatakiwa kuanza kuzungumza mbele za watu kwa sababu hicho ndicho kitu ambacho kinakuogopesha wewe.
2. Jiweke vizuri.
Kama aibu yako imekutawala sana basi hakikisha unajiweka mwili wako na mavazi katika hali ya uzuri na nadhifu, kama ni mavazi basi vaa mavazi ambayo watu hawatakutolea sana macho yao, hii ni kwa sababu kama umevaa mavazi ya ajabu basi watu ni lazima watakuwa na wewe kukutazama, kitendo kitakachokufanya ujisikie aibu, hivyo kila wakati ili uondokane na aibu jiweke mwenyewe katika hali ya uzuri.
3. Jifunze kwa watu wengine ambao hawana aibu.
Najua katika mazingira ambayo unaishi wewe wapo baadhi ya watu huwa hawaana aibu kabisa, hivyo unachotakiwa kufanya ni kuhakikisha unajifunza kutoka kwao kwamba wao huwa wanafanyaje hadi kutokuwa na aibu, ikiwezekana waulize huenda wakakupa mbinu mbalimbali za kuondokana na aibu.
4. Vuta pumzi ndefu.
Kama aibu yako ni kwamba huwa unashindwa kuzungumza mbele za watu basi unachotakiwa kufanya ni kuhakikisha kuwa unafanya zoezi fupi kabla ya kuanza kuzungumza na zoezi hili si jingine bali ni kuvuta pumzi ndefu kabla ya kuanza kuzungungumza mbele za watu, pia unapozungumza usipende kumuangalia mtu muda mrefu machoni pake maana atakufanya upotezee kujiamini kwako.
5.  Anza mazoezi ya kuzungungumza.
Anza kufanya mazoezi ya kuzungumza, anza kuzungumza ukiwa peke yako ili ukifika mbele za watu iwe ni kitu cha kawaida tu, mazoezi ya kuzungumza wanashauri wakati unaanza ni vyema ufanye mazoezi katika kioo ambacho kitakuonesha unazungumza. Kioo ni njia nzuri sana katika kujijengea uwezo wa kujiamini.
Mpaka kufikia hapo sina la ziada, nikutakie siku njema, endelea kutembelea Muungwana blog kila wakati.

Jinsi ya kutumia sekunde tatu kumtongoza mwanamke

Habari za muda huu mdau na mfuatiliaji wa makala mbalimbali zinazokujia kupitia mtandao huu wa Muungwana Blog bila shaka umzima wa afya na unaendelea vyema na majukumu yako ya kila siku.
Naomba nichukue walau dakika zako chache kuweza kukujuza mbinu hii ya sekunde tatu kuweza kumtongoza mwanamke yule umtakaye na endapo utatumia sekendu hii tatu mwanamke huyo ni lazima atakuwa wako.
Sekunde tatu ni sekunde za maangamzi dhidi yako na yule unayemuona mbele yako. Endapo ukimwona mwanamke ambaye unataka kumtongoza, kwa kawaida kuna zile sekunde tatu za kwanza ambapo unafaa uchukue hatua kabla ile sauti ambayo inajaribu kuongea na wewe kukuzuia kufanya hivyo.
Tunasisitiza uchukue hatua ya kuweza kumtongoza mwanamke huyo ndani ya sekunde tatu kwani ukishindwa kufanya hivyo basi mwanamke huyo atapita bila ya wewe kuweza kufanya hivyo.
Kila mwanaume akichelewa kuapproach mwanamke kuna ile sauti ambayo inaanza kukuongelesha kwamba sijui hamna kitu hapo, hii ndiyo ile sauti ambayo inawafanya wanaume wengi wabaki kuwa single milele.
kwahiyo la kufanya hapa ukimwona mwanamke unayetaka kumuapproach basi fanya fasta. Una sekunde tatu za kuweza kufanikisha mpango mzima la sivyo kila msichana mzuri anayepita mbele ya macho yako utaendelea kumuita shemaji.

Unamtongoza, Anasema Anakuchukulia Kama Rafiki, Unajua Kwanini?

Stori inakwenda hivi; baada ya kumwangalia kwa muda mrefu, huyumwanamke anambae anakuuwa pole pole kwa mvuto wake, ambae anakila kitu ambacho wewe macho yako kwako unaona ndo kile kinachoitwa na kutengeneza uzuri usiopimika, ubongo wako unaamini ya kuwa mnaendana kwa kila kitu ila kinachokuchanganya ni wewe kutokua na uhakika iwapo na wewe unampendeza yeye, Kijana wa watu unajituma na kupiga moyo konde, leo hii unajikaza kiume na kwenda kumwambia yale yote yaliyo moyoni mwako… mara… ‘kwaaa…’ anakujibu, “Oho, lakini mbona mie siku zote huwa nakuona na kukuchukulia kama rafiki, kama rafiki.. rafiki tu!”, moyo unapigwa na radi ya maumivu, na huamini kilichokupata, huku kichwani sauti ya “kama rafiki” ikijirudia rudia!.
Kama kungekua na kitu cha kuzuia hii dhihaka, ungetumia na kurudisha muda nyuma, kiume.com tumekusanya dalili zote za kuangalia kabla ya kupiga moyo kode na kwenda kumwambia yanayokusibu moyoni…
Anajiamini sana akiwa na wewe mpaka mazoea yake yamepitiliza…Msichana akiwa anajiamini sana kwako, ujue hapo umeshapoteza unachotamani na umeishia kunawa, kwa msichana akimuona mtu anayempenda kweli, utaona dalili…!, utaona hatulii, mara akae vizuri, na anakua anajihisi tu mda wote, atashika nywele zake kuangalia kama ziko vizuri, mapenzi asikuambie mtu kaka, mapenzi yanaleta kutokujiamini, na iwapo anajiamini sana kwako na ashtuki akikuona, wala atikisi hata ukucha basi hapo tafuta kitu kingine tu cha kufanya.
Anakupa hadithi za wanawake wengine… Msichana ambae yupo singo hana mpenzi, halafu ukiwa nae anakua anakupa stori za wasichana wengine, hapo anatumia janja ya nyani, hapo anakubadilisha akili usimwazie yeye na uwawazie hao wasichana wengine anaokupigisha stori, achana kabisa na haya maongezi, anaweza kukwambia.. “ooho, unaonaje nikikupigia pande kwa rafiki yangu Janeti, si ni mzuri eeh?”, kaka hapo unapoteza mda tu.
Hafanyi kile unachotaka…Ukiona msichana hasikilizi kile unachotaka, yeye siku nzima anakuomba umsaidie hichi, twende pale.., we ukimwambia ya kwako anaruka maili tisa, ujue hapa huna chako, we upo pale ili akutumie tu na kwa sababu hana hisia nawe hajiulizi hata huyu jamaa anajisikiaje!.
Anatukana bila kujari uwepo wako…Maneno anayotumia ni kama yupo namwanamke mwenzie, na wala hashituki!, kaka hapa umeshakwenda na maji, mapenzi yana heshima na anayekupenda huwa anashituka akiona tu uwepo wako, na aibu yake sikuzote hua ipo karibu.
Hataki kuonekana na wewe sehemu za wazi…Ukimwambia tutoke wote, anakua na visingizio. Ukimwambia twende wote nikusindikize uendako, hata kama ni sokoni… utamsikia “ohhoo, mi nilishazoea kutembea mwenyewe wakati wote, mama atanielewa vibaya”. Hapa ni kwamba anaogopa utamwalibia chansi ya kukutana na mwanaume wa ukweli achana na wewe masuruali tu, mama gani ambae hapendi mwanae aolewe?.
Anakuomba misaada mda wote…  Msichana mwenye hisia nawe hawezi kukuomba misaada ovyo hovyo, kwanza atakua hajiamini na hujiuliza maswali kama “Hivi atanionaje na atajifikiliaje nikimuomba hiki?”.
Anakufanya kama spea tairi…Siku akikubali kutoka mtoko nawe, utashangaa kaja na mashoga zake!, hii anakua anafahamu kabisa kwa hio anakua anajihami ili usije ukapata chansi ya kuwa wewe na yeye. Yeye saa zote ni vicheko tu…, kidogo tu mara anaenda chooni, mwisho wa siku mbaba unaagwa usiku umeingia sie tunaenda.
hafanyi michezo yeyote ya kuwa karibu nae…Mwanamke akikupenda anatamani saa zote awe karibu nawe, mara mjikute mmeshikana mikono mda mrefu mpaka jasho, sasa huyu yeye atakua anakulia taimingi, anakua anahakikisha hakuna mguso wa ajabu ajabu, kaka mguso huleta hisia, na kama hana hisia kwako hawezi kufanya hivyo.
Anaongea na wanaume wengine mbele yako…Hivi hili si linaonekana kabisa, hili halina haja hata la kuliongelea, ila mtu akiwa amependa inawezekana kabisa asilione hata hili, anakua anajipa matumaini hewa!, huku kichwani akilipa sababu nyingine kabisa, “Oooh yuko sosho sana!”.Kaka hapo kama msemo wa kiumeni.com usemavyo, “umeshaliwa kekundu”.
Hakutambulishi kwa rafiki zake…Hana hisia nawe atakutambulisha kwa nini?, labda kwa sababu vocha zote zinatoka kwako!, samahani kwa kuongea hivi najua nakukera ila ndo ukweli wenyewe, na hata ukitambulishwa, utatambulishwa kama rafiki tu, na hivyo ndo utabaki kuwa.
Cha kufanya jiongeze, na hata kama yeye ndo huwa anakupigia simu au anakufata na anaonyesha hisia ujue kuna kitu zaidi ya wewe kinachoendelea kumweka kwako.

NJIA YA KUMTONGOZA MWANAMKE AWE MPENZI WAKO

Kuna baadhi ya wanaume hawajui jinsi ya kuzungumza na mwanamke au msichana. Kwa njia hii wanaume wengi wanaishi maisha ya bila kumvutia mwanamke yeyote. Hapa kuna njia 10 utakazozitumia wewe mwanaume ili kuhakikisha humkwazi mwanamke unayempenda mnapokuwa katika mazungumzo nae…
 
1. Wakati ukizungumza nae, jaribu kuzungumzia “hisia” kama vile kumbu kumbu yako ya utotoni, matarajio ya baadae au matamanio yake. Mada hii ya mazungumzo yenu yatafungua milango ya hisia zake ghafla.
 
2. Wanawake huhitaji mwanaume asiyekuwa na uoga wa kuwamiriki na kuwaongoza. Wakati unazungumza na mwanamke tawala mazungumzo yenu, kamwe usimpe nafasi ya yeye kuanza kufikiri, kuwa nini uchokuwa ukizungumza.
 
3. Kuwa makini wakati unapokuwa ukizungumza naye kwa majibu yasiyo na anayokuwa akikujibu, na kama kwa bahati mbaya ukonaye karibu kiasi cha kugusana, basi jisogeze pembeni wakati ukiwa unaendelea kuongea ili asishtukie au unaweza kumuona hayuko sawa katika utoaji majibu… kwa kawaida atakuonyesha ishara, hivyo kuwa nazo makini.
 
4. Kumbuka hii kauli mbiu “Ucheshi/vituko si mapenzi”. Wanawake huvutiwa sana na wanaume wanaoweza kuwafanya wawe na furaha muda wote. Usijikite zaidi katika kufanya utani unaopita kiasi na kusahau ulichokuwa unaongea. Bali jikite zaidi katika mambo yanayomfanya ajisikie kuwa na msisimko na starehe wakati ukonae.
 
5. Zama katika undani wa mazungumzo baina yako na yeye. Mwanamke huendana na mwanaume asiyekuwa muoga wa kuzungumzia mambo binafsi kwa ukaribu.
 
6. Wanawake wengi hupenda kujua maoni yako kuhusiana na jinsi unavyomuona. Mwambie vitu unavyoviona kutoka kwake, lakini jaribu kuwa makini ili usitamke vitu vingine vitakavyo msababishia apoteze furaha.
 
7. Epuka kumpa ofa nyingi mwanamke, mwanamke huwa na mashaka na mwanaume anayempatia vitu vingi kwa wakati mmoja ama kila mara. Kwasababu atafikiri vitu unavyompatia ni kutaka kumvutia tu ili umpate kiurahisi. Kitu ambacho baadae kitaleta madhara makubwa.
 
8. Kama unahitaji kujua njia nzuri ya kuweza kuongea na mwanamke au msichana bila kumfanya asichikie au kuboreka, basi usitumie njia ya kumuuliza maswali mengi katika mzungumzo yenu. Bali cha zaidi jaribu kueleza mawazo yako kuhusu vitu flani.
 
9. Kumbuka kauli juu ya kuuliza maswali: Badala ya kumuuliza “wewe umekulia wapi?”, uliza “unaonekana kama hujakulia maeneo haya!” Hii itakusaidia wewe kufanya uchunguzi juu yake bila yeye kujua.
 
10. Usifiche utambulisho wako – zungumza vitu kutoka katika hisia zako, onyesha uhalisia wako katika kuzungumza na usitumie mikogo ya mtu yeyote.
 
Njia bora ya kufikiria jinsi ya kuzungumza na mwanamke, ni kutambua njia sahihi ya mazungumzo ya furaha na yakimahaba utakayopenda kuitumia, usimuige mtu. Kuzungumza na mwanamke si vigumu bali nikujua ni vitu gani hasa mwanamke hapendi kuvizungumzia na vitu gani anapenda kuvisikia. Fuata maelekezo hapo juu utaona matunda yake… kisha rudi utoe maoni yako.
 
MUHIMU: Maelekezo haya yote yatafanikiwa kwa mwanamke mwenye kuhitaji mapenzi ya kweli – yani sio kwa wanawake wanaolenga kuchota pesa kwako na kutokomea. Hivyo kuwa makini sana