MBINU 10 BORA ZA KUMPATA MWANAMKE MSTAARABU


JAMBO ipo msomaji wa mimi? Leo nakupakulia mbinu 10 bora zaidi za kumpata mwanamke mstaarabu, wa kukufaa na asiye kicheche. Kifupi unakuta mwanaume ana status nzuri tu lakini anakosa mwanamke anayejielewa.yaani wengine hadi wananiuliza sometimes mimi "Hivi wewe ulimpataje wanawake wako na alivyo mstaarabu vile?"

Sio lazima mpaka uwe na pesa nyingi, uwe msomi sana au uwe na kazi nzuuuuri ndo utafanikiwa kumpata mwanamke wa moyo wako, nooo, tena A BIG NO!

Hizi ni mbinu 10 bora zilizopitishwa na SHIRIKA LA NDOA HALALI BORA DUNIANI (SHINDOBODU) zinazoweza kukusaidia kumpata shemeji yetu ambaye ni hitaji la moyo wako na mwisho wa siku akawa siyo tu mke bora na mwema kwako, bali mama bora wa watoto wako, mwalimu wa jamii wa na kiongozi bora wa taifa letu.

Bofya hapa!

1: Omba namba ya simu kwa ustarabu, usitumie papara
Unapoomba namba ya simu hakikisha huombi kwa papara, yaani usioneshe kama una shida sana na usioneshe kama unataka kumtongoza, bali onesha kama unataka tu urafiki wa kawaida,yaani rafiki wa kuchati nae tu kawaida.

2: Usimtafute kila mara kwa siku za mwanzo
Akikupa namba leo kausha usimtafute leo leo, mtafute baada hata ya wiki,msalimie tu na umpigie, hapa uangalie na muda ambao unadhani mtu anakuwa free, sio kupiga simu asubuhi sana au mchana au usiku sana, piga mida ya saa mbili usiku,na usiongee nae zaidi ya dakika 5.

3: Mtumie message na kumpigia simu ambazo hazina kharaha
Hakikisha kila siku unamtumia msg mara 3 na kumpigia simu mara moja, yaani asubuhi mtakie asbh njema, mchana, jioni na usiku piga kumpa pole na heka heka za mchana, ongea nae si zaidi ya dakika 5 ili usimchoshe.

4: Tumia maneno yenye staha wakati wa maongezi
Hakikisha hutumii maneno ya mtaani sana mfabo oya,inakuwaje,michongo vipi, barida, mzuka, poa n.k. Tumia maneno mazuri ya busara mfano sawa, haya, umeshindaje, habari yako, n.k. yaani asikuone wewe hujitambui.

5: Jenga naye urafiki
Weka nae urafiki wa kudumu kiasi kwamba awe anakumiss, na ukim-text asipojibu mtumie vocha hata ya buku. Ila angalia usitumie pesa sana.

Omba outing nae, na akikubali basi mpeleke sehemu tulivu yenye adabu na sio mnaenda bar, mkiwa huko ongelea zaidi maisha ya kawaida ya mwanadamu, usiongelee ishu za X wako kamwe, ishu za mapenzi usiongelee kabisa, weka vistory vya kuchekesha ili awe anafurahi na kukumiss mkitoka hapo.

6. Mtangulize Mungu mbele.
Hata rais wetu, JPM anapenda kuutumia huu msemo, "Kila jambo unalofanya mtangulize mungu mbele".
Unapodhamiria kumpata umpendae, ni kheri ukimshirikisha Mungu wako, jikabidhi kwa Mungu na umuombee mema huyu unayetaka awe wako. Mtumie meseji zenye ujumbe wa Mungu, mkumbushe mambo ya ibada, mambo ya kumcha Mungu, kwa upole na unyenyekevu mkubwa, sio lazima uanze kumhubiri nooo! Tafuta pointi 2 au 3 muelekeze vyema.

7: Ongea kwa vituo, usiongee kama cherehani
Ukiwa unapiga nae stori kwenye simu usiwe unaongea sana, na hata mkiwa pamoja basi usiongee sana kama chiriku, pangilia maneno sana ya kuongea (waza kabla ya kusema).

8. Kuwa mcheshi
Nadhani unafahamu ya kuwa njia ya kumvutia mwanamke lazima utumie lugha ya ucheshi mara kwa mara. Well, uzuri ni kuwa si lazima uwe na ustadi wa kuchekesha.
Unaweza kuelezea matukio yako ya awali ambayo uliona yalikuchekesha. Kama mwanamke anaonyesha dalili za kukupenda, basi kila neno utakalolitoa kiutani atacheka.

9. Msifie kadri uwezavyo
Unaweza kumsuka kwa kutumia mizaha wakati ambapo mko na marafiki zenu. Lakini wakati ambapo mko nyinyi wawili, tumia maneno ambayo hatayasahau kiurahisi. Mfano unaweza kumwambia "wewe ndie unafanya siku yangu kuwa ya shangwe", "kukaa na wewe hapa najiskia niko huru" nk kutamfanya yeye kujiona spesho kwako.

Ujanja hapa ni kutumia maneno ambayo yatamfanya yeye kujiona spesho kuliko yeyote na amini usiamini mwanamke kama huyu atakuwa akifikiria mazungumzo yenu kwa muda mrefu.

10. Jitahidi kuwa bora zaidi kuliko wanaume wengine
Katika dunia tunayoiishi sahizi kila mwanaume anatamani kuwa na mwanamke bora zaidi. Hivyo kutaka kuwa na mwanamke unayempenda lazima uwe bora kuliko wengine.

Hii ni kuanzia tabia zako, vile unavyohusiana na wengine, miondoko yako, unadhifu wako nk. Kuwa mwanaume bora hakuna njia ya mkato. Lazima ufuate mkondo ambao wengi hawaufahamu.

Baada ya urafiki wa kama miezi miwili hivi, hapo sasa mtamkie wazi wazi kwamba unampenda tangu muda mrefu, na umtongoze kwa heshima sana. Nakuhakikishia hapo hachomoki hata kwa dawa.

NOTE: Mbinu hizi ni za kumpata mwanawake anayejielewa, anayetaka mwanaume/mpenzi na sio anayetaka pesa.
Kwa wale wanawake vicheche, we tumia pesa tu, ukimtongoza leo jioni basi kesho ni wako.

Post a Comment

أحدث أقدم