MANENO MATAMU YA MAPENZI YA KUMWAMBIA MSICHANA.

 


Kwa hili naamini maneno matamu, wakati ule unapokuwa unajaribu kupata msichana umtakae maishani mwako ili uuteke moyo wake awe wako, unahitaji kujifunza  jinsi ya kutumia  maneno matamu
. Lakini ukumbuke si kila neno linaweza kuugusa moyo wa mwanamke. Lakini maneno matamu  hufanya vitu vya kushangaza sana , humtoa nyoka pangoni.
Wakati wanaume wengine wanalalamika  ni jinsi gani ilivyo vigumu kuuteka moyo wa msichana, jibu ni rahisi sana , ni kwa sababu hawatumii  maneno sahihi. Watu wengi pia wanakosa maneno, wengine hata hawajui  wapi  pakuanzia  na wataanzaje,  ngoja tuanze na haya maneno yafuatayo, maneno matamu ya kumwambia  msichana.
1.Macho yako ni mazuri sana, yananivuta, nashindwa  la kufanya, lakini  yananifanya nipotelee kwako.
2.Unanifanya niwe mwanaume bora, kwa hio naweza kustahili kwenye  penzi letu.
3.Unaonekana mzuri kama malaika,  nahisi nikikushika nitakuchafua.
4.Napatwa na woga ndani ya tumbo langu , natetemeka unapoweka mikono yako juu ya uso wangu.
5.Umefanya ndoto zangu ziwe za kweli.
6.Sijawahi kukutana mtu mzuri na mwenye kujali kama wewe.
7 Nakupenda sana, kiasi kwamba siwezi kujielezea hata kama nikijaribu.
8 Wewe ni msichana mzuri  ambae  kamwe  sikuwahi kukutana nae.
  1. Unafanya  huzuni zangu kupotea  kwa tabasamu lako zuri.
  2. Hapana, wewe sio mnene, uko poa na ndivyo nipendavyo.
11.Ungeweza kupata mwanaume yeyote ulimwenguni na bado umenichagua mimi.
12.Unanipa maana ya maisha yangu.
13.Sitaki kufikiria maisha yangu bila wewe katika hili.
14.Unakuaje mzuri muda wote?
15.Unanifanya nijione mwenye bahati ninapokuwa na wewe.
16.Magoti yangu huishiwa nguvu kila nikugusapo.
17.Wewe ni rafiki yangu wa kweli,  najifunza kwako, na ni mtu ambae najua nitakuwa nawe, ni mpenzi wa maisha yangu, niwewe tu nilienae. Ni kila kitu kwangu.
18.Siwezi kuamini kama mtu mwema kama wewe usingeweza kuwa na mimi.
19.Sijui kama unaelewa kiasi gani ninavyokupenda.
20.Natamani niwe na wewe maisha yote, lakini  muda hautoshi wa kukupenda vya kutosheleza.

Post a Comment

Previous Post Next Post